Leo Jumamosi kumefanyika kikao cha waratibu na walezi TAYOMI-CASFETA NA BCF, kikao kimefanyika katika chumba cha mikutano kanisa la PHM kadege kuanzia saa 3:00asubuhi hadi Saa 9:00 alasiri.
Kikao hicho kimefana sana kikiongozwa na mratibu wa Mkoa C.G Kasalile na katibu Ask. Kazio pamoja na waratibu wengine Mwl.Nsojo, Mama mratibu wa BCF, Mhandisi Angumbwike na RTS Mgogo. Wajumbe walikuwa waratibu wa ngazi zote pamoja na walezi wa matawi mbalimbali ya CASFETA na BCF wakiwemo waratibu wapya ambao wamehitimu CASFETA akiwemo Mwl Veronica, Mwl Patrick, Dada Vaileth na wengineo wakiwemo walezi wasio na mipaka na vinguke wa CASFETA mkoa wa Mbeya Ndg Kapagi Mwl Mkongwe wa kwaya Dada Salome.
Kikao kilikuwa cha aina yake kwa kukutanisha mazao ya CASFETA watumishi ambao hawajaonana muda mrefu.
Ajenda mbalimbali zimejadiliwa zikitiwa chachu na ya Kambi la Pasaka, Umiliki wa uwanja pamoja na mikakati ya kuundeleza pamoja na ile ya account ya mkoa.
Maazimio muhimu ni pamoja na kuyafikia matawi mbalimbali kukagua uhai wa matawi hayo ikiwemo kuhamasisha mahudhuria ya kambi la Pasaka.
Mkoa wa Mbeya umejiandaa kufanya makambi matatu ya Pasaka katika vituo vya Jiji la Mbeya, Rungwe na Mbalali.
Bwana anatufanikisha sana kazi yako ni kupiga magoti na kuipeleka mikakati hii mbele ya Mungu kwa maombi.
No comments:
Post a Comment